Ticker

6/recent/ticker-posts

Bao la 100 la Marcus Rashford Lasaidia Man Utd Kuizamisha West Ham

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

Bao la 100 la Marcus Rashford lilisaidia Manchester United kutwaa ushindi wa 1-0 dhidi ya West Ham siku ya Jumapili, Oktoba 30. 

Rashford ni mmoja wa wachezaji wa Mashetani Wekundu walioimarika zaidi msimu huu baada ya miaka kadhaa ya kujiburuta. 

West Ham bado hawajashinda ugenini dhidi ya United kwenye Ligi Kuu Uingereza wakipoteza mechi 12 kati ya 16 walizoshiriki. 

Rashford ndiye alikuwa kifaa muhimu kwa United na alivamia safu ya ulinzi ya West Ham kwa shuti kali lililomgonga Craig Dawson na kuruka juu ya lango.  

Bila kufa moyo Rashford alijaribu kuonja wavu tena kwa kichwa akiunganisha krosi ya Diogo Dalot na kumlazimu kipa wa West Ham Lukasz Fabianski kuchukuwa hatua ya kuipangua. 

Fowadi huyo Muingereza alirejesha matumaini ya mashabiki wa United katika dakika ya 38 ambapo alipita kati kati ya Thilo Kehrer kupatana na krosi ya Christian Eriksen na kutia kimyani akiwa hatua ya sita akitumia kichwa. 

Rashford aliendeleza mashambulizi katika kipindi cha pili akijaribu kutafuta bao la pili bila kufua dafu. 

Cristiano Ronaldo ambaye pia alichezeshwa kwenye mechi hiyo, aliwachwa akikuna kichwa baada ya kupoteza nafasi mbili za wazi za kufunga mabao. 

Wakiwa hawajapoteza katika mechi nane zilizopita katika michuano yote, United sasa wako na pointi moja nyuma ya Newcastle walio katika nafasi ya nne katika mbio za kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa msimu ujao. 

Post a Comment

0 Comments