Ticker

6/recent/ticker-posts

M-Bet yaijaza mabilioni Simba, waipiku Yanga

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa


KLABU ya soka ya Simba imesaini mkataba wa miaka mitano na kampuni ya kubashiri ya M-Bet kama mdhamini mkuu wa klabu hiyo wenye thamani ya billioni 26.1.

Mkataba huo umesainiwa  leo Agosti Mosi mwaka huu, ambapo umeifanya klabu hiyo kuwa ndio yenye thamani kubwa katika klabu zote zitakazoshiriki Ligi Kuu kwa msimu ujao.

Kwenye mkataba huo katika kipindi cha mwaka wa kwanza, Simba kiasi cha shilingi 4.6470, kwenye mwaka wa pili watapokea kiasi cha shilingi bilioni 4.925.

Kiasi hicho cha fedha kitaendelea kuongezeka kwenye mwaka wa tatu Siba itapewa kiasi cha  shilingi bilioni 5.205, na mwaka wa nne watapewa shilingi bilioni 5.514 na mwaka wa tano ambao ndio wa mwisho wa mkataba watapewa shilingi bilioni 5.853.

Mkataba huo ni mkubwa kuliko ule waliosaini wapinzani wao klabu ya Yanga, siku chache zilizopita na kampuni ya kubashiri ya Sports Pesa wenye thamani ya shilingi bilioni 12 kwa kupindi cha miaka mitatu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, Barbara amesema  M-Bet ni kampuni kubwa ya kubashiri Tanzania na imewekeza katika klabu kubwa Tanzania na Afrika Mashariki na ndio maana wamesaini mkataba huo.

“M-Bet imekidhi mahitaji yetu, huwezi kuona wanaenda sehemu nyingine kuweka udhamini katika klabu za hapa’’  amesema Barbara na kuongeza;

“Mkataba wetu na M-Bet ni upande wa timu ya wakubwa tu, timu za vijana na wanawake hauhusiani mkataba huu, labda kama tutafungua ukurasa mpya".

Barbara ameongeza akisema, ”Wadhamini wetu wote wanne wamejipanga vilivyo kuisapoti timu yetu ndani na nje ya nchi.

Kampuni hiyo inaingia kama mdhamini mkuu wa klabu hiyo baada ya kumaliza mkataba wake na Sportpesa na mgawanyo wa fedha utakuwa kama ifuatavyo;

Mwaka wa kwanza - Sh4.670 bilioni

Mwaka wa pili - Sh4.925 bilioni

Mwaka wa tatu - Sh5.205 bilioni

Mwaka wa nne - Sh5.514 bilion

Mwaka wa tano - Sh5.853 bilioni.

Jumla ni Sh26,168,5000 ya mkataba huo kwa miaka mitano ndani ya Simba.

Kwa upande wa wadhamini hao ambao waliwakilishwa na Allan Mushi amesema kuwa mkataba huo wenye thamani ya shilling bilioni 26.1 kwa mda wa miaka mitano na wameungana na Simba kwa kuwa ni klabu kubwa nchini Tanzania na inawakilisha vizuri nchi kuimataifa.

“Sisi kama M-Bet tuna amini kuwa tukishirikiana vizuri na Simba tutajitangaza ndani na nje ya Tanzanania maana Simba ni timu kubwa” Alisema Mushi

Pia mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi  ya Simba Abdallah amesema Simba inawashukuru wadhamini waliopita na sasa wapo na wadhamini wa wapya pia milango ipo wazi kwa makampuni maana bado kuna Simba queens na timu za vijana sababu Simba ni klabu ya watu wako tayari kufanya kazi na watu wote , pia akiwashukuru M-Bet na kuwaahidi watakipata walichokitaka maana wametoa pesa nyingi

“M-Bet mlichokitaka mtakipata , pesa ni nyingi hizi tumieni hii nafasi ya mtaji wa mashabiki wetu kutanua biashara yenu” Alisema M/kiti huyo wa bodi

Aidha pia mkurugenzi wa michezo ya kubahatisha amepongzea mkataba huo na kuisisitiza M-Bet kufanya kazi kwa makini ili izidi kupata mikataba mingi na kuendelea kuiheshimisha michezo ya kubahatisha kwa ujumla.

Huu ni mkataba wa kwanza wa Simba wa udhamini mkuu wa klabu aambao wamesaini, toka walipoingia kwenye mfumo wa mabadiliko ya uwendeshaji wa timu katika kipindi cha miaka mnne iliyopita.

Post a Comment

0 Comments