Ticker

6/recent/ticker-posts

Muonekano wa jezi mpya za Azam fc

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

Muonekano  wa Jezi Mpya Ya Azam fc Msimu Ujao 


BAADA Ya Yanga hapo jana kutambulisha Jezi zake kwa ajili ya msimu Ujao wa Ligi, Leo Klabu ya Azam fc imezindua JEZI zake mpya ambazo zinatarajiwa kutumika kwa msimu wa 2022/23.

Azam FC wamezindua jezi za msimu ujao 2022/23 leo Ijumaa (July 29) kwa kuzionesha kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii.

Mbali na kufanya hivyo, kwenye kurasa za mitandao ya kijamii, pia wamezindua kupitia Azam TV kwenye kipindi cha Alasiri Lounge.

Azam FC inajiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara pamoja na Michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF).

Azam Fc immezindua jezi za nyumbani,ugenini na zile za tatu Jezi za nyumbani zitakuwa ni za rangi nyeupi,za ugenini rangi ya bluu na zile za tatu rangi ya nyeusi.

Jewzi hizo zitaanza kuuzwa katika maduka ya timu hiyo na ya vifaa vya michezo kwa gharama ya Tsh 22,000 kwa jezi moja.








VIDEO: ‘MTOKO’ WA TAIFA: Huu hapa ‘uzi’ wa nyumbani wa Azam FC kuelekea msimu mpya wa 2022/23.
VIDEO:MTOKO’ WA TAIFA: Huu hapa ‘mtoko’ namba tatu (third kit) wa Azam FC kuelekea msimu mpya wa 2022/2023

Post a Comment

0 Comments