Ticker

6/recent/ticker-posts

KOMBE LA DUNIA LA FIFA: Mataifa Manane Ambayo Yamewahi Kushinda Kombe la Dunia

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

Mashindano ya Kombe la Dunia yaliandaliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1930 nchini Uruguay wenyeji wakiibuka washindi kwa kuwavyoga Argentina. 

Tangu kuasisiwa kwake, Kombe la Dunia limeandaliwa kila baada ya miaka minne (Qatar 22 yakiwa makala ya 22) na kushindwa na mataifa manane pekee. 

Je, mataifa hayo ni yapi? 

1. Brazil - mara tano 

Brazil ilifika fainali 1950 lakini ikavunjwa moyo kwao nyumbani na Uruguay waliobuka bingwa. 

Mwaka 1958 hata hivyo, nyota ya jaha iling'aa kwa Samba Boys wakiwatandika wenyeji Uswidi 5-2 katika fainali na kushinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza. 

Brazil ilifanikiwa kutetea taji hilo miaka minne baadaye katika makala ya 1962 yaliyoandaliwa nchini Chile kwa kulima Czechoslovakia 3-1 katika fainali. 

Samba Boys walitemwa nje katika hatua ya makundi mwaka 1996 lakini wakarejea miaka mmine baadaye na kushinda taji lao la tatu kwa kutandika Italia 4-1 katika fainali nchini Mexico. 

Miamba hao wa Amerika Kusini walilazimika kusubiri hadi makala ya 1994 yaliyoandaliwa nchini Marekani kabla ya kupapasa tena kombe hilo kwa kuwanyuka Italia 3-2 kwa penalti kufuatia sare tasa baada ya dakika 120. 

Mara ya mwisho Brazil kushinda Kombe la Dunia ni katika makala ya 2002 yaliyondaliwa katika mataifa ya Korea na Japan. 

Ronaldo alifunga mabao mawili na Samba Boys kulaza Ujerumani 2-0 katika fainali. 

2. Ujerumani - mara nne 

Ujerumani - kwa wakati huo ikiitwa Ujerumani Magharibi iliibuka bingwa kwa mara ya kwanza mwaka 1954 kwa kutoka mabao mawili nyuma na kunyuka Hungary 3-2 katika fainali nchini Uswizi. 

Wajerumani walishinda Kombe la Dunia kwa mara ya pili walipokuwa wenyeji mwaka 1974 kwa kunyuka Uholanzi iliyoongozwa na Johan Cruyff 2-1 kwenye fainali. 

Mwaka 1990, Ujerumani ilishinda Kombe la Dunia kwa mara ya tatu kwa kuinyuka Argentina 1-0 katika fainali ugani Olympic jijini Rome nchini Italia. 

Tukio hilo lilijirudia mwaka 2014, Mario Gotze alipofunga bao la ushindi katika dakika 30 za ziada na Ujerumani kunyuka Argentina 1-0 katika fainali iliyoandaliwa nchini Brazil.


3. Italia - mara nne 

Italia ilishinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 1934 ambapo ilikuwa mwenyeji kwa kunyuka Czechoslovakia 2-1 katika fainali iliyoelekea katika muda wa ziada. 

Miaka minne baadaye nchini Ufaransa, Italia ilikuwa taifa la kwanza kutetea taji hilo kwa kuitandika Hungary 4-2 katika fainali. 

The Azzurri ilihitajika kusubiri jadi mwaka 1982 ili kutwaa taji lake la tatu kwa kuipiga Ujerumani 3-1 katika fainali iliyoandaliwa nchini Uhispania. 

Katika makala ya 2006 yaliyoandaliwa nchini Ujerumani, timu zote zikiwa sare ya 1-1 baada ya muda wa ziada, Italia iliipiku Ufaransa 5-3 kwa mikwaju ya penalti na kushinda Kombe la Dunia kwa mara ya nne.

4. Argentina - mara mbili 

Argentina ilifika fainali ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 1978 ilipoandaa mashindano hayo. 

Wenyeji hao waliwatandika Waholanzi 3-1 baada ya muda wa ziada na kushinda kombe hilo kwa mara ya kwanza. 

Albiceleste - wanavyofahamika kwa jina lao la kimajazi - ilishinda Kombe la Dunia kwa mara ya pili mwaka 1986 nchini Mexico baada ya kuinyuka Ujerumani kwa usaidizi wa nyota Diego Maradona. 


5. Ufaransa - mara mbili 

Ufaransa iliandaa mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 1998 ya kunyima Brazil nafasi ya kutetea taji hilo. 

Les Bleus waliwanyuka Samba Boys 3-0 katika fainali na kushinda kombe hilo kwa mara ya kwanza. Wafaransa walilazimika kusubiri miaka 20 kabla ya kutwaa ubingwa wa kombe hilo kwa mara ya pili - wakitandika Croatia 4-2 katika fainali iliyoandaliwa nchini Urusi. 


6. Uruguay - mara mbili 

Uruguay ilikuwa mwenyeji wa makala ya kwanza ya Kombe la Dunia mwaka 1934 na ikaibuka bingwa kwa kuitandika Argentina 4-2 katika fainali. 

Timu hiyo ilitokea kushinda kombe hilo kwa mara ya pili mwaka 1950 ilipotoka nyuma na kuwalima waandalizi Brazil 2-1 kwenye fainali. 


7. Uingereza - mara moja 

Uingereza imeshinda Kombe la Dunia mara moja - makala ya mwaka 1966 ambayo ilikuwa mwenyeji. 

The Three Lions waliwatandika Wajerumani 4-2 baada ya muda wa ziada katika fainali iliyoandaliwa ugani Wembley, jijini London. 


8. Uhispania - mara moja 

Baada ya kufulia katika Kombe la Dunia kwa miaka mingi, hatimaye Uhispania ilishinda Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza mwaka 2010 nchini Afrika Kusini. 

Andres Iniesta alifunga bao la kipekee katika muda wa ziada na Uhispania kuizamisha Uholanzi 1-0 katika fainali. 

Post a Comment

0 Comments