Ticker

6/recent/ticker-posts

KOMBE LA DUNIA FIFA 2022: Giroud, Mbappe Waiongoza Ufaransa Kuitandika Australia 4-1 Kwenye Kombe la Dunia

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

Olivier Giroud aliweka historia ya Thierry Henry kama mfungaji bora wa mabao wa Ufaransa baada ya kufunga mabao mawili katika mechi dhidi ya Australia. 

Mabingwa watetezi walianza kampeni yao ya Kombe la Dunia kwa ushindi wa 4-1 Jumanne, Novemba 22. 

Australia ndiyo walichukua uongozi wa kushtukiza kwenye Uwanja wa Al Janoub kunako dakika ya tisa wakati Craig Goodwin alipowaweka kifua mbele alipounganisha krosi ya winga Mathew Leckie. 

Ufaransa, ambao kikosi chao kilikumbwa na mizimwi ya majeraha, walimshuhudia beki Lucas Hernandez akiondoka mapema uwanjani kwa sababu ya jeraha hali iliyochangia bao hilo la Australia. 

Hata hivyo, walisawazisha bao hilo kupitia kwa kiungo wa kati Adrien Rabiot akitumia kichwa kunako dakika ya 27 kisha baadaye alichangia bao la kwanza la Giroud katika dakika ya 32 ikiwa ni bao lake la 50 katika mashindano ya kimataifa. 

Kylian Mbappe pia alijijengea jina katika kipindi cha pili akichangia bao la pili la Giroud katika dakika ya 71 na kufikia rekodi ya Henry ya mabao 51 kwa Ufaransa na kufanya mambo kuwa 4-1. 

Giroud hakufunga bao kwenye michuano ya Kombe la Dunia makala ya mwaka wa 2017. 

Mapema, Mbappe alikuwa amefunga bao kwa kutumia kichwa akimalizia krosi ya Ousmane Dembele. Mbappe alifanya mambo kuwa 3-1 katikati ya kipindi cha pili.

Ushindi huo unawaacha Ufaransa kileleni mwa Kundi D baada ya wapinzani wao Denmark na Tunisia kutoka sare tasa. 

Post a Comment

0 Comments