Ticker

6/recent/ticker-posts

Frenkie De Jong Asema Hakutamani Hata Kidogo Kujiunga na Man United

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

  • Kiungo wa Barcelona Frenkie de Jong amefichua kuwa hakutaka hata kidogo kujiunga na Manchester United 

  • Mustakabali wa de Jong Camp Nou ulikuwa haujulikani lakini akagoma kuungana tena na kocha Erik ten Hag 

  • Beki Antonio Rudiger aishangaa Chelsea kumfukuza kocha Thomas Tuchel 


Kiungo wa Uholanzi Frenkie de Jong amefichua kuwa hakutaka hata kidogo kujiunga na Manchester United katika dirisha la uhamisho lililopita licha ya mustakabali wake katika klabu ya Barcelona.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 25 alionekana kuwa njiani kuondoka Camp Nou huku akidai Barcelona malimbikizi ya mshahara kwa kima cha yuro milioni 17. 

“Nilitaka kubaki Barcelona na ndio maana nilisalia mtulivu kaika dirisha la uhamisho. Siwezi kusema mengi kuhusu hilo,” De Jong alisema katika kikao na waandishi wa habari akiwa na timu ya taifa ya Uholanzi. 

United ilimtaka sana De Jong kocha Erik ten Hag akilenga kuduma zake lakini kiungo huyo wa Oranje alipambana kwa udi na uvumba kusalia Barcelona. 

“Klabu ilikuwa na mipango yake name pia nilikuwa na mipango yangu. Wakati mwingine mipango hukinzana lakini mwisho wa siku mambo yalienda vyema,” De Jong aliongeza. 

Rudiger aishangaa Chelsea kumtimua Thomas Tuchel 

Beki wa Real Madrid Antonio Rudiger ameelezea mshangao wake baada ya kuona kocha Thomas Tuchel akitimuliwa na klabu ya Chelsea. 

Rudiger alitumika kama mchezaji wa akiba chini ya kocha Frank Lampard lakini Tuchel alipotua Stamford Bridge, alitokea kuwa ngome kwa the Blues. 

Na baada ya kuondoka mwishoni mwa msimu kwenda Real Madrid kama mchezaji huru, Rudiger ameshangazwa na waajiri wake wa zamani kumpiga kalamu Tuchel. 

“Kwanza aliruhusiwa kuleta wachezaji wapya, kisha akatimuliwa baada ya mechi chache. Nilishangazwa na kasi hiyo. Siku ya kutimuliwa kwake ilikuwa huzini kwangu. Nilimwandikia ujumbe baadaye na kumshukuru tena kwa kila kitu,” Rudiger aliambia shirika la Sport1.

Post a Comment

0 Comments