Ticker

6/recent/ticker-posts

Man United Yaitandika Liverpool Mbele ya Umati Old Trafford

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

  • Mashabiki wa nyumbani walifurahia burudani Manchester United ikiwazamisha maadui wao Liverpool mbele ya ummati 

  • Huu ndio ushindi wa kwanza kwa Man United msimu huu wa EPL na wa kwanza kwa kocha Erik Ten Hag nchini Uingereza 

  • Man United imejizoa kutoka mkiani kwa sasa ikishikilia nafasi ya 14 kwa alama tatu huku Liverpool ikiwa kwa bano la timu sita za mwisho 

Klabu ya Manchester United imeibuka na ushindi wa bao 2-1 dhidi ya mahasimu wa jadi Liverpool katika mechi ya Ligi Kuu ya Uingereza maarufu kama EPL jijini Old Trafford mnamo Jumatatu, Agosti 22.


Ujasiri wa Erik Ten Hag 

Kocha wa Manchester United Erik Ten Hag alifanya maamuzi wa ujasiri akiwaacha kwenye benchi nahodha Harry Maguire na mshambuliaji nyota Cristiano Ronaldo katika mechi hiyo muhimu. 

Ten Hag pia aliamua kuwapa Raphael Varane, Tyrell Malacia na Anthony Elanga mwanzo wao wa kwanza msimu huu huku pia sajili mpya kiungo Casemiro kutoka Real Madrid akitambulishwa kwa mashabiki. 


Mabao ya Man United na Liverpool 

Dakika chache baada ya Elanga kugonga chuma, alimwandalia pasi wing'a wa Uingereza Jadon Sancho aliyewapa United uongozi katika dakika ya 16. 

Mechi hiyo ilielekea mapumzikoni United wakiwa uongozini, kocha Ten Hag akimwondoa Elanga mwanzoni kwa kipindi cha pili na kumpa nafasi Anthony Martial. 

Dakika nane baadaye, Martial alimpakulia pasi Marcus Rashford aliyefanya mambo kuwa 2-0 kwa faida ya mashetani wekundu. 

Mohamed Salah aliwagungia Liverpool bao la kufuta machozi katika dakika ya 81. 


Ushindi wa kwanza wa United na Ten Hag 

Huu ndio ushindi wa kwanza kwa United msimu huu wa EPL na wa kwanza kwa kocha Erik Ten Hag nchini Uingereza tangu kuchukua mikoba Old Trafford. 

United imejizoa kutoka mkiani kwa sasa ikishikilia nafasi ya 14 kwa alama tatu huku Liverpool ikiwa kwa bano la timu sita za mwisho.

Post a Comment

0 Comments