Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa
Manchester United wanakaribia kumsajili Lisandro Martinez kwa pauni milioni 46.5 ($55m). Mazungumzo na Ajax sasa yako katika hatua za mwisho.
United
ilijiweka kwenye nafasi nzuri kwa Martinez baada ya wapinzani wao, Arsenal,
kurudi nyuma kwa imani kwamba mchezaji huyo alipendelea kuhamia Old Trafford.
Ajax walihofia kumuuza - wakikataa dau la awali la karibu £40m ($47m). Lakini mchezaji
huyo wa kimataifa wa Argentina aliweka wazi kuwa anataka kuhamia Premier League
na kuungana na Ten Hag, ambaye alikuwa meneja wake na mabingwa hao wa Uholanzi(Ajax).
United
walisubiri kufikisha nia yao ya kumnunua Martinez lakini walijua kuwa ada ya
kati ya £45-50m ingetosha kupata mkataba baada ya kuona ofa za chini kutoka kwa
Arsenal zimekataliwa.
Nia ya
mchezaji huyo kuungana na Ten Hag pale Old Trafford. Na huu utakuwa usajili wa
pili kwa meneja Erick Ten Hag.
0 Comments