Ticker

6/recent/ticker-posts

Ousmane Dembélé Kubaki Barcelona hadi 2024

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

Ousmane Dembélé Kubaki Barcelona hadi 2024



Ousmane Dembélé Atasaini mkataba mpya wa kuendelea kuitumikia Barcelona baada ya mazungumzo ya muda mrefu kukamilika. 


Ousmane atasaini mkataba utakao mwezesha kusalia Barcelona mbaka mwaka 2024, ni mkataba wa miaka miwili. Mkataba huo unapitiwa na wanasherika na unatarajiwa kusainiwa wiki hii.  


Dembélé amekubaliana na vipengele vyote vilivyomo kwenye mkataba wake baada ya Barcelona kufanya maboresho, rasmi amezipiga chini ofa zote kutoka vilabu vingine. 


Dili hili ni muhimu kwa kocha Xavi Hernández, kwa sababu ndiye aliye mshawishi mchezaji huko kubaki na pia ni shabiki wake mkubwa na  bado anamuhitaji aendelee kusalia Barça kama sehemu ya mipango yake ya baadae.

Post a Comment

0 Comments