Ticker

6/recent/ticker-posts

Mohamed Salah Alikuwa Tayari Kujiunga na Chelsea Kabla ya Liverpool Kumpa Dili Nono

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

 Mohamed Salah Alikuwa Tayari Kujiunga na Chelsea Kabla ya Liverpool Kumpa Dili Nono


Kiungo wa Liverpool Mohamed Salah alikuwa anawazia kujiunga na Chelsea kabla ya kuweka mkataba mpya wa miaka mitatu na klabu hiyo Salah alijiunga na Chelsea mwaka 2014 akitokea Basel lakini alikuwa na wakati mgumu London kabla ya kuuzwa AS Roma Liverpool walimpa Salah ofa bora zaidi ya mkataba mrefu huku vilabu vikubwa kama vile Chelsea vikimezea mate huduma zake 

Mohamed Salah anaripotiwa kwamba alikuwa tayari kujiunga tena na Chelsea kabla ya Liverpool kumpa ofa mpya na bora zaidi. Mohamed Salah alikuwa anawazia kujiunga na Chelsea kabla ya kuweka mkataba mpya wa miaka mitatu na klabu hiyo.

Ripoti za awali zilisema kwamba Salah hakuwa na budi kuachana na Liverpool kwa klabu nyingine ya Ligi Kuu iwapo hatapata kandarasi yake anayotaka Anfield. Liverpool ilishangaza wengi ilipomfanya Salah kuwa mchezaji anayepokea kitita kizito zaidi kwenye Ligi Kuu ya Uingereza katika mkataba wake mpya wa miaka mitatu. Reds wanadaiwa kuvutiwa na Chelsea kutaka kumnunua Mmisri huyo kama Sports Mole inavyoripoti 

Kikosi cha Jurgen Klopp hakikuwa tayari kumpoteza mchezaji mwingine nyota baada ya Sadio Mane kuondoka klabuni na kusajiliwa na Bayern Munich. Nia ya Chelsea ilionekana kuwa kubwa ikizingatiwa kuwa klabu hiyo inahitaji kuhimarisha safu yake ya ushambulizi. Iwapo uhamisho huo ungekamilika, Salah angejiunga tena na klabu ambayo aliichezea kati ya 2014 na 2016. Muda wake katika klabu ya Chelsea ulikuwa wa hali ya chini kwani alishiriki mechi 13 pekee za EPL. 

Aliuzwa AS Roma kabla ya kurejea na kujiunga na Liverpool. Katika mkataba wake mpya na Reds, fowadi huyo Mmisiri sasa atakuwa akipokea akipokea KSh50 milioni kwa wiki sawa na KSh200 milioni kila mwezi. Salah alikuwa amesalia na miezi 12 pekee katika mkataba wake wa awali na Reds. Mchezaji huyo mwenye uzoefu anajivunia rekodi ya kufungia Liverpool mabao 156 kutoka kwa mechi 254 tangu ajiunge na klabu hiyo mwaka wa 2017 akitokea AS Roma ya Italia. 

Vile vile ameshinda mataji kadhaa ikiwemo ya UEFA, EPL, Kombe la FA, FIFA Club World Cup, UEFA Super Cup kwa kipindi cha miaka mitano akiwa Anfield. 

Post a Comment

0 Comments