Ticker

6/recent/ticker-posts

Arsenal Yakamilisha Usajili wa Oleksandr Zinchenko Kutoka Man City

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

 Arsenal Yakamilisha Usajili wa Oleksandr Zinchenko Kutoka Man City

  • Oleksandr Zinchenko amejiunga rasmi na Arsenal akitokea Manchester City kwa kima cha pauni milioni 30 
  • Beki huyo wa timu ya taifa ya Ukraine ametia wino mkataba wa miaka mine ugani Emirates 
  • Ni mchezaji wa tano kusajiliwa na Arsenal katika dirisha hili la uhamisho na tayari ameshajiunga na kikosi nchini Marekani



Beki wa timu ya taifa ya Ukraine Oleksandr Zinchenko amekamilisha uhamisho wake kutoka mabingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) Manchester City na kutua Arsenal. 

Zinchenko mwenye umri wa miaka 25 amesaini mkataba wa miaka minne Emirates baada ya kujiunga na klabu hiyo kwa ada ya Uhamisho wa pauni milioni 30. 

Beki huyo anajumuika tena na Mikel Arteta ambaye alikuwa kocha msaidizi wa City kabla ya kuchukua mikoba ya kuinoa Arsenal. 

“Tuna furaha Alex amejiunga nasi. Ni mchezaji ninayemjua binafsi na nimeendelea kumfuatilia hata baada yangu kutoka Manchester City. Alex ni mchezaji wa viwango vya juu na atatufaa katika idara mbalimbali. Nimefurahishwa kwamba kila mmoja amefanya juhudi kubwa kumleta Alex katika klabu hii,” Arteta amesema. 

Zinchenko alijiunga na Manchester City mwaka 2016 akitokea Ufa FC ya Urusi na amechezea the Citizen mechi 128 na kuwafungia mabao mawili. 

City imemshukuru na kumtakia heri njema katika taaluma yake baada ya kushinda mataji manne ugani Etihad, manne yakiwa ya EPL. 

“Kujiunga na Manchester City kulibadili maisha yangu na nitashukuru daima kwa nafasi niliyopewa. Ni klabu ya kipekee na muda wangu hapa umekuwa wa kipekee,” Zinchenko aliambia tovuti ya mancity.com.

Beki huyo wa kushoto ni mchezaji wa tano kusajiliwa na Arsenal katika dirisha hili la uhamisho baada ya Gabriel Jesus, Marquinhos, Matt Turner na Fabio Vieira kutua Emirates. 

Tayari amejiunga na kikosi cha timu hiyo Orlando nchini Marekani kwa maandalizi ya msimu mpya huku nambari yake ya jezi ikiratibiwa kutangazwa baadaye. 

Post a Comment

0 Comments