Ticker

6/recent/ticker-posts

Simba Sc Kuikabili Mbeya Kwanza Jumatano Mjini Songea

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa

 

Baada ya Simba Sc Kupoteza mechi yao siku ya jana dhidi ya Tanzania Prisons sasa yaelekea Songea Kuikabili Mbeya Kwanza Siku ya Jumatano.

Kikosi chetu kimeanza safari asubuhi hii kuelekea mjini Songea tayari kwa mchezo wa Jumatano wa kukamilisha msimu wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mbeya Kwanza.

Kikosi kimeondoka jijini Mbeya baada ya mchezo wa jana kwa basi kikiwa na wachezaji wote tuliosafiri nao kwa ajili ya mechi mbili za Nyanda za Juu Kusini.

Baada ya timu kuwasili Songea wachezaji watafanya mazoezi ya utimamu wa mwili (recovery) baada ya mechi ya jana dhidi ya Tanzania Prisons na kesho tutafanya ya mwisho.

Mchezo wetu dhidi ya Mbeya Kwanza utapigwa Jumatano saa 10 jioni katika Uwanja wa Majimaji.

Je,Unatafuta Ajira? Bofya hapa Kutuma Maombi


Post a Comment

0 Comments