Ticker

6/recent/ticker-posts

Majina Ya Form Six Waliochanguliwa Kujiunga Na JKT Awamu Ya Pili

Kwa maombi ya kazi, Bofya hapa


 


Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), limetoa siku tatu kwa vijana walioitwa kuhudhuria mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa kuripoti makambi ya JKT mara moja.

Pia JKT imetoa nyongeza ya majina ya vijana waliohitimu elimu ya kidato cha sita mwaka 2022 kujiunga na mafunzo ya JKT kwa mujibu wa sheria kwa mwaka 2022.

Haya yameelezwa jijini hapa na Mkuu wa Tawi la Utawala JKT, Brigedia Jenerali, Hassan Mabena alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu wito wa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Mujibu wa Sheria mwaka 2022 Awamu ya Pili.

Alisema Mkuu wa JKT, Meja Jenerali Rajabu Mabele anawataka kuripoti makambini vijana wote walioitwa kuhudhuria Mafunzo ya JKT Kwa Mujibu wa Sheria kwa mwaka 2022, ambao hawajaripoti mpaka sasa waripoti makambi ya JKT mara moja.

Alisema vijana hao wanaotakiwa kuripoti makambi ya JKT yaliyo karibu na maeneo wanayoishi.

Bofya Hapa >>>>JKT Form Six SECOND Selections 2022 | List of Selected Students to Join JKT 2022 National Service

Post a Comment

0 Comments